« Mahdi or Messiah »






SWAHILI

Bismillahir rahamanir rahiim

Sema ukweli umedhihiri, uongo umejitenga

Mirza Ahmad Qadiani, ndiye Mahdi au Masihi aliyeahidiwa?

Na. Dk. Rashid

Assalaam Alaykum

Uislamu dini ni teule ya Allah; Qur'an ni ujumbe wa mwisho wa Muumba kwa Wanaadamu ulioletwa kupitia Mitume wake na Mtume wa mwisho katika mlolongo wa mitume hao ni Muhammad(SAW).

Katika hadithi kadhaa, Mtume ameripotiwa kusema kwamba yeye ni Mtume wa mwisho wa Allah(SW). Mtume Muhammad alibashiri juu ya kuja kwa Mahdi(a.s) na kuja tena kwa Nabii Issa kabla ya kiyama.

Hata hivyo, katika kipindi cha miaka 1400 iliyopita wamejitokeza wadanganyifu wengi ambao wamekuwa wakitoa madai ya uongo kuhusiana na nyadhifa hizi tatu; Mtume, Masiha na Mahdi. Katika wadanganyifu hao Mirza alidai kuwa yeye ni Mtume, yeye ni Masih na yeye ni Mujadid(Muhuishaji wa Uislamu).

Makala hii fupi itachunguza madai yote haya matatu kwa kutumia Qur'an na Hadithi za Mtume kwa ajili ya manufaa ya Waislamu wote hasa wale wasio na mwanga mzuri wa mafundisho ya Uislamu ambao pamoja na kutomuona wala kumsikia Mirza lakini wametumbukia kiupofu kufuata itikadi yake kutokana na harakati za kundi la Ahmadiyya.

Uislamu - Dini teule ya Allah

Mwenyezi anatufahamisha katika Qur'an:

"Leo hii nimekamilisha ujumbe wangu kwenu na nimekuchagulieni Uislamu kuwa dini yenu(njia yenu ya maisha)(5:3)

Kuhusiana na Mtume Muhammad(s.a.w)

Allah anatufahamisha kuwa Muhammad(s.w) ndiye Mtume wa mwisho na hakuna Mtume mwingine baada yake:

"Muhammad si baba wa yetote miongoni mwa wanaume wenu bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na Muhuri(mwisho) wa Mitume na Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu(33:40).

Mtume Muhammad katika hadithi kadhaa ameweka wazi zaidi kwamba yeye ndiye Mjumbe na Mtume wa mwisho wa Allah(s.w), na hakuna mtume wmingine baada yake. Baadhi ya Hadithi hizo ni:

Mtume amesema: "Wana wa Israil waliongozwa na Mitume. Kila Mtume alipotawafu, aliinuliwa Mtume mwingine kushika nafasi hiyo. Lakini baada yangu hakuna Mtume mwingine; watakaofuata baada yangu ni Makhalifa.(Bukhari, Kitab al Manaqib).

Katika Hadithi nyingine Mtume ameripotiwa kusema: Nafasi yangu katika mlolongo wa mitume walionitangulia inaweza kufafanuliwa na mfano ufuatao:

"Mtu amejenga nyumba na kuinakshi vizuri lakini ikawa kwenye kona moja likakosekana tofali moja.. Watu wakaajabia uzuri wa nyumba hiyo lakini wakashangazwa na kukosekana tofali katika kona hiyo. Mimi ninafanana na tofali hilo na mimi ni wa mwisho katika mlolongo wa Mitume". (Bukhari, Kitab Manaqib)( Kwa maneno mengine kuinuliwa kwa Mtume Muhammad(s.a.w) kunakamilisha haja ya utume, ameziba mwanya unaoweza kuhitajia kuja kuzibwa na mtume mwingine).

Kadhalika Mtume(s.a.w) amesema: Mwenyezi Mungu amenifadhilisha mimi katika mambo sita ambayo mitume wengine hawakufadhilishwa mambo hayo ni:

1. Nimetunukiwa urahimu na ufasaha wa kusema

2. Nimebarikiwa uwezo wa kuwashinda maadui

3. Nimehalalishiwa kupigana vita

4. Ardhi yote imefanywa mahali pa kufanyia ibada kwangu na imefanya kuwa ya kujitaharishia. Kwa maneno mengine katika dini yangu swala haukufungiwa iwe inafanyika amahali maalum pa ibada. Swala ya kuswaliwa mahali popote twahara katika Ardhi hii. na yanapokosekana maji inajuzu kuchukua udhu kwa kutumia udongo(kutayamamu) na kujisafisha miili kwa kutmia udongo inapotokea uhaba wa maji.

5. Nimetumwa na Allah kupeleka ujumbe kwa ulimwengu mzima. Na

6. Mlolongo wa Mitume wa Allah kwa Wanaadamu umekomea kwangu

Mtume(s.a.w) amesema: Mkufu wa wajumbe na Manabii umekamilika baada ya kuja kwangu. Hakutakuwa na Mtume atakayekuja baada yangu"(Tirimidh, Kitab-ur Rouya babu Zahab-un - Nubuwwa, Musnad Ahmad, Marwiyat- Anas bin Malik)

Mtume(s.a.w) amesema: ”Mimi ni Muhammad, Mimi ni Ahmad, mimi ni mfutaji, ukafiri utafutwa kupitia mafundisho yangu; mimi ni mkutanishaji. Watu watakutanishwa siku ya mwisho baada yangu(Kwa maneno mengine kitakachokuja baada yangu ni simu ya hesabu). Mimi ni mwisho kwa maana kwamba hapana mtume atakayekuja baada yangu"(Bukhari na Muslim, Kitab al Fadhaail, Bab: Asmaun Nabi; Tirmidh, Kitab ul Adab, Bab: Asma un Nabi; Muatta, Kitab u Asmain nabi, Al Mustdrak Hakim, Kitabul Fitan, Bab: Dajjal).

Abdur Rahman Bin Jubair ameripoti: Nilimsikia Abdullah Bin Amr ibn Al As akihadithi kwamba siku moja Mtume alitoka nje ya nyumba yake na kujumuika nasi. Kwa jinsi alivyoonekana ilikuwa kama anatuaga. Akasema:

"Mimi ni Muhammad, sijui kusoma wala kuandika ni Mtume wa Mwenyezi Mungu' akarudia mara tatu kusema hivyo. Kisha akatamka: hapatakuwa na Mtume mwingine baada yangu"( Musnad Ahmad, Marwiyat Abdullah bin Amr ibn-As).

Mtume(s.a.w) alimwambia Ali kwamba, Wewe unahusiana na mimi kama vile ilivyokuwa kwa Harun na Musa(a.s). Lakini hapatakuwa na Mtume baada yangu". (Bukhari na Muslim, Kitab Fadhail as Sahaba).

Thauban ameripoti kwamba: Mtume(s.a.w) amesema: Kutaibuka wadanganyifu thalathini katika umma wangu na kila mmoja kati yao atautangazia ulimwengu kuwa yeye ni Mtume, lakini jueni kwamba mimi ndiye wa mwisho katika mlolongo wa Mitume wa Allah na hakuna Nabii atakayekuja baada yangu".(Abu Dawud, Kitab ul Fitan).

Mtume(s.a.w) amesema: Hakuna Mtume atakayeinuliwa baada yangu na kwa hiyo hapatakuwa na wafuasi wa Mtume mpya baada yangu"(Baihaq, Kitab ul Rouya; Tabaran).

Mtume(s.a.w) amesema: Mimi ni wa mwisho katika mlolongo wa Mitume wa Allah na Msikiti wangu(akiashiria msikiti wa Madina) ndio wa mwisho".(Muslim, Kitab ul Hajj; Bab: Fadl us Salat bi Masjid Makka wala Madina).

Kutokana na Hadithi hizi sahihi, itakuwa wazi kwa msomaji kwamba hakuna Mtume baada ya Muhammad. Hata hivyo akionesha kupuuza kabisa maelezo hayo ya Mtume, Mirza Ghulam Qadiani ni miongoni wa waliodai kuwa ni Mitume wa Allah. Mirza ametamka wazi wazi kuwa yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu matamshi ambayo ni kinyume kabisa na mafundisho ya Qur'an na Hadithi za Mtume(s.a.w).

Ni nani atakayekuwa Imam Mahdi kama ilivyobashiriwa katika Ahadithi za Mtume Muhammad(s.a.w).

Dai jingine la Mirza Mwasisi wa Kundi la Ahmadiyya ni kwamba yeye ndiye Imam Mahdi. Waislamu wengi wameonekana kutekwa na dai hili. Hebu tutazame Mtume(s.a.w) nini amesema kuhusiana na kuja kwa Imam Mahdi.

. Neno halitafutika mpaka mtu miongoni mwa familia yangu, ambaye jina lake litakuwa jina langu, atakayewaongoza Waarab wote(Tirmidh Sahihi, juzuu ya 9, uk. 74; Abu Dawud, Sahihi, juzuu5, uk.207; vile vile imeripotiwa na Ali bin Abi Talib, Abu Sai'd , Um Salma, Abu Huraiyra).

. Kabla ya siku ya Hukumu, Allah atamleta kutoka mafichoni Mahdi anayetokana na Familia yangu. hata kama itakuwa imebaki siku moja ya maisha haya ya ulimwengu atapigania Haki na usawa katika ardhi hii na ataondoa ufisadi na ukandamizaji. (Musnad Ahmad Ibn Hanbal, juzuu ya 1, uk. 99).

Walau itabaki siku moja kabla ya kiama, bado Allah atampeleka mtu kutoka katika familia yangu atakayepigania kusimamisha haki na usawa, hata kama ukandamizaji huo utakuwa umeenea kiasi gani katika ardhi.(Abu Dawood).

. Masih aliyeahidiwa atatoka katika ukoo wangu katika nasaba ya Fatima(Binti wa Mtume). (Sunan Ibn Majah, juzuu 2., hadithi na. 4086.

. Mahdi ni mmoja kati yetu, ni miongoni mwa Ahlul Bayti. (Sunnan Ibn Majah, juzuu 2, hadithi na. 4085.

Kwa mujibu wa hadithi nyingi sahihi na zinazokubalika za Mtume(s.a.w) Imam Mahdi ameelezwa:

1. 1. Atatokana na ukoo wa Mtume(s.a.w) na kizazi cha Fatima

2. 2. Atakuwa na uso wa bapa na pua ya kuchongoka

3. 3. Atatokea usiku mmoja

4. 4. Atakuja muda mfupi kabla ya kiama

5. 5. Atafanana jina na Mtume(s.a.w)

6. 6. Atakimbia kutoka Madina kwenda Makka ambako watu watampokea na kula kiapo mbele yake

7. 7. Atapokea kiapo na kuwasaidia watu wa Iraq

8. 8. Atapigana vita.

9. 9. Ataongoza sehemu kubwa ya Waarabu kwa mujibu wa sunna kwa muda wa miaka saba

10. 10. Ataeneza haki na usawa katika ardhi

11. 11. Ataondoa ufisadi na ukandamizaji

12. 12. Hatakuwa yule masihi aliyeahidiwa

Je Mirza Ghulam Qadian alifikia vigezo na kukamilisha majukumu haya?

Hadithi zinazoelezea juu ya ujaji wa Issa bin Maryam

Mirza amedai kwamba yeye ndiye Masihi aliyeahidiwa yaani Issa bin Maryam aliyebashiriwa na Mtume(s.a.w) atakayekuja kabla ya siku ya kiama. Alikuwa sahihi kwa madai yake haya? Hebu tutazame Mtume(s.a.w) amesemaji kuhusiana na hili:

"Naapa kwa yule mikono yake inamiliki uhai wangu, Mwana wa Maryam(Issa) atatoa Talbiya(Labbaika Allahumma Labbaika) kwa ajili ya Hajj, au Umra au yote kwa wakati mmoja katika mlima wa Rawha."(Sahih Muslim, kitabu cha 7, Na. 2877).

Mwenyezi Mungu atamtuma Masih Ibn Maryam. Atashukia jirani na mnara mweupe wa mji wa Damascus, akiwa amevaa shuka mbili za njano, akiwa juu ya mabega ya malaika wawili.(Sahih Muslim, juzuu ya 8. uk. 192-193.

Masih atakufa baada ya kukamilisha muda aliokadiriwa kuishi hapa duniani na Waislamu watamswalia na kumzika jirani na kaburi la Mtume, Abubakar na Omar."(Mishkat, uk.480).

Mujammi Ibn Jariya al-Ansar ameeleza kwamba alimsikia mtume(s.a.w) akisema: Mwana wa Maryam atamuua mpinga Kristo(Dajjal) katika lango la Ludda.(Tirmidh na Ahmad).

Kwa mujibu wa hadithi hizi sahihi yafuatayo yanafahamika:

1. 1. Masihi aliyeahidiwa si mwingine ila ni Issa bin Maryam

2. 2. Atakuja kuwa miongoni mwa Waislamu, atashukia jirani na mnara mweupe ulioko Damascuss, Syria, akiwa amejigubika shuka mbili za njano akiwa katika mabega ya malaika wawili.

3. 3. Ataswali nyuma ya Imam Mahdi

4. 4. Atapambana na kumuua Dajjal katika lango la Ludd;

5. 5. Masiha atatawala na kuongoza dola ya kiislamu kwa mujibu wa sharia ya Qur'an

6. 6. Watu wa kitabu watakiri kuwa Issa ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu na watasilimu(4:159), watavunja misalaba na jizya kwao itaondolewa.

7. 7. Atapambana na Yaajuj na Maajuj na atashinda vita hivyo

8. 8. Uislamu na Haki vitatawala, ukandamizaji utaondoshwa na vita sehemu mbali mbali vitamalizwa.

9. 9. Kila mtu atapata kipato kinachomtosha na chuki, wivu na tamaa vitafutika

10. 10. Masih atahiji au atafanya Umra

11. 11. Atakufa baada ya kuishi duniani kwa muda wa miaka 40 na atazikwa jirani na kaburi la Mtume. Kuja kwake kutakuwa alama mojawapo ya kiama.(43:61).

Je Mirza ametimiza masharti haya ambayo Mtume ameapa kuwa yatatokea.

Je, Mirza Ghulam Ahmad alikuwa; Mtume au Masih aliyetabiriwa au Imam Mahd?

Mirza hakuwa Mtume au Mahdi wala Masih aliyetabiriwa bali alikuwa:

. Mtoto wa Chirag Bibi, na si mtoto wa mwana wa Maryam

. Hatokani na ukoo wa Mtume(s.a.w)

. Hakupata nafasi ya kutawala nchi na kusimamisha haki.

Mirza Qadiani anakiri mwenyewe:

."Sijadai kwamba mimi ni Mahdi atakayekuja ambaye atatokana na ukoo Fatima"(Braheen-e-Ahmadiyya V. Roohani Khaazin juzuu ya 21 uk. 356).

."Tunakiri hivi kwa sababu huenda wakaja Mahdi wengi siku za usoni na huenda mmoja wao akawa na jina la Imam Muhammad."(Roohani Khazain juzuu ya 3 uk. 197).

."Inawezekana na kwa hakika muda fulani huko mbeleni atakuja mtu Takayeitwa Masih ambaye ni yule aliyebashiriwa na Mtume, kwa sababu mimi siku mtawala na sikuwa na amri katika ulimwengu huu bali nilikuwa *****ara na mnyonge.

."Huenda wakaja Masih zaidi ya 10,000 na wa kweli akawa yule atakayeshukia Damascuss.(Izala -e-Auham), Roohani Khazain juzuu ya 3 uk. 251).

Kwa hiyo Mirza alijijua kwamba yeye si Imam Mahdi wala mcha Mungu yeyote aliyebashiriwa na Mtume, licha ya hivyo wafuasi wake wameendelea kusisitiza kwamba alikuwa Imam Mahdi. Na kama kweli alikuwa Imam Mahdi basi alishindwa kutimiza majukumu aliyotakiwa kuyafanya kwa mujibu wa hadithi. Licha ya kujua kwamba madai yake yanapingana kabisa na mafunzo ya Mtume Muhammad, tamaa ya ya kishetani ilimsukuma Mirza afumbie macho dhambi kubwa aliyokuwa akiitenda. Alihalalisha madai yake kwa kusema:

"Msingi wa madai yetu sio Hadithi, ni Qur'an na Wahyi niliokuwa nikiupokea. Ndio, na katika kuthibitisha hili ningeonesha Hadithi ambazo kwa mujibu wa Qur'an hazipingani na Wahyi wangu. Hadithi nyingine nazitupilia mbali kama karatasi isiyohitajika."(Roohani Khazain juzuu ya 19. uk. 140).

Ni wazi kabisa mwasisi wa kundi la Ahmadiya ametoa madai yanayopingana kabisa na Quran. Maulamaa wa Makka, Madina, Cairo na Ulimwengi mzima wa kiislamu wametangaza ya kuwa hawa ni Murtad na kwa hivyo ni Makafiri si miongoni mwa makundi ya kiislamu. Mirza na wafuasi wake ni waasi wanaotakiwa kupigwa vita na Waislamu wote duniani. Mirza alikufa miaka 100 na kidogo iliyopita lakini wafuasi wake wangalipo wanaendelea kudanganya watu kwa jina la Uislamu.

Ujinga unaotokana na kukosa mafunzo sahihi ya Uislamu na mafunzo potofu ya Mirza Ghulam Ahmad ni matunda ya harakati za wamishenari. Ni jukumu la kila Muislamu kuulinda Uislamu dhidi ya udanganyifu wa Murtadi hawa. Muislamu asikubali kutumbukia kwenye uongo wa Ahmadiyya kwa sababu ya ujinga. Mafunzo ya Uislamu yako bayana, afanye hima kuyajua. Ifahamike kwamba mtu anapoamua kujiunga na Murtadi hawa ajue amekufuru. Ukweli uko bayana na uongo uko bayana. Hakuna kulazimishwa mtu katika mas'ala ya dini.

Mwenyezi Mungu awalinde Waislamu kutokana na ukafiri unaoenezwa na harakati za Ahmadiyya kwa kuyapotosha mafunzo ya Uislamu.

Ewe Mwenyezi Mungu warejeshe kwenye Uislamu Waislamu waliozugwa na Uhamadiyya. Wawezeshe kulijua lipi la kweli na lipi la uongo na wape hidaya ya kufuata njia iliyo sahihi. Amiin.

Wamaa alaina illal balaagh

Hatukuwa sisi ila wafikishaji

Wassalaam alaykum

Kundi la Harakati za kupinga Uhamadiya

P.o.Box 11560

Dibba, AlFujaira

Muungano wa Falme za Kiarabu

rasyed@emirates.net.ae

http://alhafeez.org/rashid/



» تاريخ النشر: 26-11-2009
» تاريخ الحفظ:
» شبكة ضد الإلحاد Anti Atheism
.:: http://www.anti-el7ad.com/site ::.