عرض المقال :Writings Speak
  الصفحة الرئيسية » مـقـالات الموقـــع » كشف البلية بفضح الأحمدية » Non - Arabic Articles » Swahili

اسم المقال : Writings Speak
كاتب المقال: webmaster

Anti ahmadiyya Mouvement in Islam

MAANDIKO YAELEZA

Tawasifu ya Mirza Ghulam

MAISHA YA AWALI YA MIRZA QADIANI

" Uzawa wangu ulijiri mwaka 1839 au 1840 A.D. Mimi nilikuwa pacha.

Pacha mwenzangu alikuwa msichana ambaye jina lake lilikuwa jannat

(pepo). Katika ufunuo wangu ‘Ya Adam uskun antaa wa zaujuka’, ambao

ulitajwa katika Brahiin Ahmadiyya ukurasa wa 496, miaka 20 iliyopita, neno

hili ‘jannat’ lilibeba maana hii maalum kwamba msichana aliyezaliwa pacha

na mimi, jina lake lilikuwa jannat ambapo msichana huyu alikufa baada ya

kuishi miezi 7"

Tiryq-ul-Quluub, Roohani Khazain Juz.15 uk. 479 na Mirza Ghaulam Ahmad Qadiani).

"Baba yangu Mirza Ghulam Murtuza alikuwa Mmiliki mashuhuri wa mashamba.

Wakati wa utoto wangu, elimu yangu ilianza kwa namna ambayo nilipokuwa na

miaka 6-7, Mwalimu wa Kiajemi aliajiriwa ambaye alinifundisha Qur’an na vitabu

vichache vya Kiajemi. Jina lake lilikuwa ni Fazl Ilahi. Wakati nilipotimiza umri wa

miaka 10, mwalimu wa Kiarabu (Moulvi) ambaye jina lake lilikuwa ni Fazl Ahmad

akaajiriwa kunifundisha. Nilipokuwa na umri wa miaka 17-18, nilipata fursa ya kupata

elimu fulani kutoka kwa baba yangu. Alinifundisha Sarufi, Mantiki na Tiba (hukmat)

ambapo baadhi ya vitabu vya tiba nilifundishwa na babaangu. Kwa sababu ya afya

yangu, baba yangu, mara kwa mara, alikuwa akinikataza kusoma-soma sana.

"Kuhusiana na vijiji ambavyo serikali ya Mwingereza ilivitaifisha, baba yangu

alifungua kesi katika mahakama ya Mwingereza ili kuvirejesha. Mimi nikateuliwa

kuwakilisha katika kesi hizi. Ingawaje jambo hili halikulingana na kimo changu na

ingawaje sikutaka kupoteza muda wangu mahali hapo pabaya lakini nilililazimika

kufuatilia mashauri hayo ya mashamba. Enzi hizo niliajiriwa na Mwingereza katika

mahakama ya Sialkot kwa miaka michache nikiwa karani kwa ujira wa Rupia 15/-kwa mwezi.

"Baadae nikajiuzulu na, kwa mara nyingine, nikapata kazi katika menejimenti ya

mashamba. Mara nyingi nilikuwa nikiitafakari tafsiri ya Qur’an. Nilipotimiza umri wa

miaka 30-35 babaangu akafariki dunia. Wakati huo mimi nilikuwa mjini Lahore.  Baada ya baba yangu kufariki dunia ndipo mfululizo wa mazungumzo na Mungu (Mukalimat-e-llahiah) ulipoanza motomoto."

(Kitab-ul-Bariayh uk 134-136, Summary of commentary (Mukhtasari wa Tafsiri) on margins , by Mirza Ghulam Ahmad Qadiani. Roohani Khazain Juz. 13 uk. 180;

TUZUK-E-AHMADI ulioandikwa katika AKBAR-AL-HAKAM QADIAN Special No, Juz.

37 Na.18519, tarehe 21-28 Mei 1934 AD).

Mirza Atoroka na Fedha za Pensheni:

"Bismillah ar- Rahmani ar-Rahiim. Bi Waalida Sahiba (Bi mkubwa yaani mamaaake

Mirza), wakati mmoja, aliniambia kuwa ‘enzi za ujana wake, Masihi Muwuud

alipokwenda kupokea pensheni ya babu yako, binamu yake aliyeitwa Mirza Imamdiin

naye alimfuata. Alipopokea pensheni, basi kwa hila na udanganyifu binamu yake

huyo, badala ya kumpeleka Mirza mjini Qadiani yeye akampeleka nje ya Qadian,

akaenda naye huku na kule na alipotumia fedha zote, Imamdiin akamtelekeza Mirza

na kutorokea mahali fulani. Masihi Muwuud hakurudi nyumbani kutokana na aibu na

kwa kuwa babu yako mara nyingi alimtaka afanye kazi , basi akafanya kazi katika Mahakama ya Naibu Kamishina wa Mji wa Sialkot kwa mshahara mdogo".

(Seeratul Mahdi sehemu ya 1 uk. 41 na Mirza Bashiir Ahmad s/o Mirza Ghulam Ahmad Qadiani)

KUANGUKA KWA FAMILIA

"Baba yangu, Mirza Ghulam Murtuza alikuwa akikalia kiti katika jumba la Gavana, na

alikuwa mpenzi wa serikali ya Mwingereza na shujaa katika moyo wake, ambapo

katika uasi wa mwaka 1857 AD, aliisaidia serikali ya Mwingereza, kwa kiasi

kilichozidi uwezo wake, alinunua farasi 50 kwa pesa iliyotoka m*****oni mwake na

kutoa askari wa kujitolea elfu hamsini. Hadhi ya mashamba tuliyomiliki ilikuwa

inashuka siku hadi siku ambapo hadi kufikia zama zetu hadhi ya familia yetu ilikuwa

ya mmiliki ardhi wa daraja la chini". (Tohfa-e-Qaiser, Roohani Khazain juz. 12

uk.270-271).

"Mwingereza alitaifisha ardhi ya familia yetu na akaweka pensheni ya heshima ya

Rupia 700/- tu kwa mwaka kwa fedha taslimu ambayo ilipunguzwa hadi Rupia 180/-

alipokufa Babu yangu na ikasita kabisa baada ya kifo cha babaangu mkubwa."

(Seerat-ul-Mahdi, Sehemu ya 1 uk.41 na Mirza Bashiir Ahmad s/o Mirza Ghulam Ahmad Qadiani)

MARADHI YA YULE ALIYEAHIDIWA

"Magego yake (Mirza Ghulam Qadian) yalikuwa na uozo ambao ulikuwa ukimletea

maumivu mara kwa mara ambapo jino moja lilichongoka na kusababisha kidonda kwenye ulimi wake, ikabidi lichongwe."

(Siirat-ul-Mahdi sehemu ya ii uk. 135 Na Mirza Bashiir Ahmad s/o Mirza Ghulam Ahmad Qadiani).

" Aliwahi kudondoka kutoka dirishani na kuumia mkono ambao ulilemaa hadi mwisho."

(Siiratul-ul-Mahdi sehemu ya ii uk. 198)

UKHANITHI

« Kikongwe huyu ana maradhi ya ulemavu wa ubongo. Kwa muda mrefu baada ya kuoa, nilikuwa nikijiona khanithi ».

(Barua ya Mirza Ghulam Ahmad tarehe: 22/2/1887 katika Makhtoobate Ahmadiyya Juz. 5, uk. 14 iliyonakiliwa kutoka Navishta-e-Ghaib by Khalid Wazirabadi)

"Wakati wa ndoa, moyo na ubongo wangu vilizorota sana na nikawa nasumbuliwa na kizunguzungu, haya yamekuwa nami kwa muda mrefu; kwa sababu ya haya, nikapata uchungu (huzuni) ya unyong’onyevu wa moyo na ukosefu wa nguvu za kiume."

(Tiryaq-ul-Quluub Roohani Khazain Juz. 15 uk 203 By Mirza Ghulam Ahmad Qadian).

Akimwandikia Hakiim Nuuruddin, Mirza kasema hivi:

"Napata nafuu kubwa kwa dawa zako. Magonjwa machache kama uchovu na asidi tumboni yametibika kwa dawa hizo. Nilikuwa na tatizo moja kubwa sana kwamba urijali wangu ulikuwa unapungua wakati nilipokuwa nikilala chini kwa ajili ya ngono. Ukosefu wa nguvu za kiume ndio uliosababisha hilo. Hivyo, kwa dawa zako nguvu zangu za kiume zimerudi."

(MAKHTOOBAT-E-AHMADIYYA Juz 5. Na. 2 Mkusanyo wa Barua za Mirza Ghulam Ahmad Qadiani).

"Wahayi ulishushwa kwangu kuhusiana na ndoa; wakati huo moyo na ubongo na mwili wangu vilidhoofu sana. Mbali ya ugonjwa wa kisukari na kizunguzungu kichwani na huzuni ya (unyong’onyevu) wa moyo, pia nilikuwa naugua kifua kikuu."

(Nuzuul-e-Masiih, Roohani Khazain juz. 18. uk. 587 tanbihi ya Mirza Ghulam Ahmad Qadiani).

" Yeye (Mirza Ghulam Ahmad Qadiani) alikuwa akifunga swaumu mara chache mwezi wa Ramadhani ambapo fidia ilitolewa; na kwa sababu ya ugonjwa, alifungua swaumu moja muda wa Magharibi. Alikuwa akipata magonjwa mara kwa mara na afya yake, kwa ujumla, ilizorota."

(Siirat-ul-Mahdi sehemu ya i uk. 51 iliyoandikwa na Mirza Ghulam Ahmad Qadiani).

"Hazrat Sahib alikuwa mgonjwa sugu wa unyogovu. Ugonjwa huu ulikuwa wa kurithi.

(Mirza Sahib hakuweza kuubeba mzigo wa Utume!!-Mwandishi). Mirza alikuwa na

mjomba wake ambaye jina lake lilikuwa ni Mirza Jamiat Baig. Alikuwa na mtoto

mmoja wa kiume na binti mmoja na wote wawili walikuwa na maradhi ya akili. Jina la

mtoto wa kiume lilikuwa ni Mirza Sher Ali. Wa kike alikuwa Hurmat Bibi. Binti huyu

akaolewa na Bwana Sahab" (Mirza na mkewe Hurmat Bibi-wote wawili machizi! Hiki lazima kiwe ni kiroja kikubwa! Na watoto waliotokana nao je?- Mtu anaweza kupata picha-Mwandishi)

(Siirat-ul-Mahdi sehemu 1 uk. 51).

UGONJWA WA UNYOGOVU KATIKA VITABU VYA KALE VYA TIBA

Unyogovu (depression), yumkini, umekuwa sehemu ya hali ya mwanadamu kwa

kipindi chote ambacho mwanadamu amekaa duniani. Hata usomaji mdogo tu wa

maandiko ya awali wabainisha maelezo juu ya unyogovu. Waandishi wa zamani

waliyatambua baadhi ya matatizo hayo ambayo sisi, baada ya miaka 2,000 hadi

4,000 ndiyo tunayatibu. Maandiko mengi ya Wagiriki yaliielezea dhanna ya unyogovu

ulioshushwa na Mungu.

Lakini miaka 2,300 iliyopita, Hippocrates alitambua kuwa matatizo ya kiakili yanatokana na sababu za kimaumbile badala ya mabadiliko ya nguvu za Kiungu.

Istilahi yake ya magonjwa ya akili bado inatumika hivi leo; epipepsy (ugonjwa wa

imani); mania (machepele), Melancholia (unyong’onyevu unaotokana na nyongo

nyeusi) na paranoia (kipaipai). Hippocrates pia kamuelezea mwanamke mmoja

aliyerukwa akili kwa unyong’onyevu ambaye alipata tatizo la kukosa usingizi, kukataa

chakula, kiu na kichefuchefu. Orodha hii ya kale ya dalili za unyong’onyevu inatoa

tahadhari kabla ya maelezo ya sasa ya ugonjwa wa unyogovu (depression).

Enzi za Warumi, daktari mmoja wa magonjwa ya binadamu, Galen, aliandika kuhusu

unyogovu. Katika kuielezea hali ya unyong’onyevu, Galen alisema kuwa wagonjwa

kadha wa kadha huonesha hofu, unyong’onyevu, kutoridhika na maisha, na kuchukia

watu wote Yeye alidai kuwa misukumo ya njozi za kufanya mambo yasiyowezekana

ilionekana katika ubongo ambao, moja kwa moja, uliathirika kwa unyong’onyevu.

Katika maelezo haya ya ensaiklopedia, Galen anajumuisha magonjwa ya dyshmia

(kisirani), crasis (khulka), na (uchepe). Kitabu cha Robert Burton, "Anatomy of

Melancholia", kilichochapishwa mwaka 1630, kilieleza kwa mukhtasari kile ambacho,

kwa wakati huo, kilijulikana kama Unyogovu na kikaainisha unyong’onyevu kama ni

"maradhi ya kichwa au akili" mara nyingi, yakinasibishwa na maumivu na huzuni.

Burton akaifagilia njia elimu ya baadae ya sayansi juu ya unyogovu na akaorodhesha

sababu za unyogovu ikiwa ni pamoja na zile za kisaikolojia kama vile aibu, soni, ghadhabu, kujipenda na kujitesa.

Mchango mwingine muhimu katika maelezo ya unyogovu ulitolewa na Freud katika

kitabu chake, Mourning and Melancholia kilichochapwa mwaka 1917. Freud aliandika

kuwa unyong’onyevu ulibainisha majuto yanayoanzia katika uchaguzi wa kitu hadi

utaratibu duni wa kujinasibisha na vitu. Maelezo yake juu ya "unyogovu wa njozi"

yanashadidia dukuduku la moyoni linalochukua nafasi ya hasira ambazo zingepaswa

kuelezwa bayana. Yeye aliamini kuwa watu wanaosumbuliwa na unyogovu hujitesa

wenyewe bila huruma huku wakiyahusisha mateso hayo na mtu mwingine kama vile

kuyahusisha na kiungo cha uzazi ambacho labda wamekipoteza. Mtu sasa anaweza

kupata picha ya kile ambacho kingemtokea Mirza kama Freud angepata fursa ya kumchunguza Mirza!

Unyogovu umeelezewa kwa maelfu ya miaka, kwanza na washairi na wanafalsafa na

hivi karibuni tu ndio umeelezewa na madaktari wa magonjwa ya binadamu. Leo hii

tumeingia katika zama ambazo maelezo kuhusu magonjwa yanachangiwa na utafiti

unaofanywa na taasisi za tiba na wanasayansi.

« Kulingana na mtazamo wa Hikmat na Ugiriki, ugonjwa huu hutokea kwa sababu ya

mkusanyiko wa nyongo nyeusi tumboni. Katika kiungo chochote inapokusanyika nyongo hii, mvuke mweusi hutokea na kupanda hadi ubongoni. Dalili zake ni:

kilungulia, kihoro cha unene hasa kwa wanawake kinachowafanya waache kula na

kuhatarisha maisha yao kwa sababu ya kudhoofu kwa tumbo, kuvurugika kwa

mfumo wa usagaji, uvimbe wa tumbo, mwendo wa hovyo, kuhisi moshi kama vile

mvuke unapanda ndani." (Je wahai na ufunuo wa Mirza ulitokana na mivuke hii?-Mwandishi). (Guide to causes & symptoms of Melancholia (Muongozo wa sababu na dalili za Unyogovu) by Allama Burhanuddin Nafees).

"Ilidhaniwa kuwa dalili za ugonjwa huu wa (unyong’onyevu) husababishwa na

udhaifu katika nguvu za kuhamasisha ngono ambazo ni ini na tumbo. Lakini utafiti

wa hivi karibuni umeonyesha kuwa huo ni ugonjwa wa akili kama vile umanyeto kwa

wanawake. Kasoro katika viungo vya ndani hupelekea katika udhaifu wa akili

unaosababisha unyong’onyevu kwa wanaume. Dalili zake: Mgonjwa mara zote huwa

mnyanyapavu wa vitu, huwa mwenye kuona wasiwasi, mara zote, akilikweza kwa

maelezo kila jambo.......huku akiwa hana hamu ya kula na uyeyushaji wa chakula

mwilini ukiwa katika hali mbaya”. (Makhzan-e-Hikmat, kilichoandikwa na Hakiim Dkt.

Gulam Jiilani).

"Usagaji hafifu wa chakula mwilini, kilungulia, sailorea, borbarigami, uvimbe tumboni,

kichomi, kuwa na uchu mbaya, kuhisi mvuke wa moshi ukipanda kichwani, dalili za

kupungua kwa unafuu wa uyeyushaji wa chakula mwilini, dalili za kuongezeka kwa

tatizo la uyeyushaji chakula mwilini, wakati mwingine, hutokea mishituko katika

viungo vya juu vya mwili, mikono na miguu na wakati mwingine mwili mzima huwa

baridi, kulingana na hatua iliyofikia ugonjwa, mwili hudhoofu, mara kwa mara mgonjwa huona miale ya mwanga mbele ya macho, mboni za macho huwa nzito, hujihisi joto na kuchomwa-chomwa kichwani na ubongoni, maumivu ya kichwa na kupaliwa kwa ghafla, zote hizi ni dalili za unyogovu."

(Akseer-e-azam, juz; 1, uk. 189 iliyoandikwa na Hakiim Mohammad Azam Khan)

Umesoma maudhui ya hapo juu kuhusu ugonjwa huu. Namuomba kila mtu, kwa

mtazamo sahihi, ayachukulie madai ya ufunuo, wahai na maongezi na Mungu

yaliyotolewa na Masihi huyu kuwa ni porojo tupu za mtu punguani na jitenge mbali na

mgonjwa huyu wa unyogng’onyevu anayeitwa mtume ili uweze kuwa Muislamu wa

kweli na kuepukana na laana ya kufuru na hivyo kuwa muumini na mfuasi mwaminifu

wa Mtume Muhammad (saw). Mtume (saw) kasema:

"Katika Umma wangu, kutakuwa na wazushi wapatao 30 na kila mmoja wao atasema

kuwa yeye ni nabii wa Mungu. Sasa ni juu yenu kubaini huyu ni mtu wa ngapi."

Sasa hebu tuone wasomi wengine wanasemaje juu ya Unyong’onyevu.

AVICENIA (ABU ALI SENA) Anasema :

"Unyong’onyevu ni ule ugonjwa ambao mawazo na fikira zisizokuwa za kawaida huzuka. Sababu yake ni kufifia kwa uchangamfu kiasi kwamba akili huruka na mgonjwa hufazaika sana kwa kufifia huko. Au kwa namna nyingine ugonjwa huu husababishwa na joto la kupita kiasi la ini. Ugonjwa huu unaitwa hypochonriasis.

Wakati uchafu wa chakula na gesi unapochanganyika katika matumbo, husababisha

kitu cheusi na pale mvuke kutoka katika kitu hicho unapopanda ubongoni, hii huitwa

unyong’onyevu wa gesi (Gaseous melancholia)"

(Canon in Medicine, Fun-e-Awwal from book 3, ABU Ali Sena (Avecina).

Tiba: Ni jambo la lazima kwa mgonjwa wa unyong’onyevu kujishughulisha na kazi ya

kuufanya moyo wake uridhike na azunguukwe na watu wa kumpa heshima na

kumliwaza. Kiasi kidogo cha mvinyo iliyochanganywa na maji kitolewe kwake kwa

wastani."

(Canon in Medicine by Avicena)

Tanbihi : Mirza Ghulam Ahmadi Qadiani alikuwa akitumia mvinyo ya toniki na afyuni kwa sababu hiyo.

"Unyong’onyevu ni mabadiliko ya fikra kutoka katika hali ya kawaida kutokana na hofu na maradhi. Kwa baadhi ya wagonjwa ugonjwa huendelea kiasi kwamba mgonjwa hudhani kuwa anaweza kuzungumzia mambo ya ghaibu na mara nyingi huzungumzia nini kitakachotokea siku za usoni. Baadae ugonjwa huu huendelea katika kiwango ambacho mgonjwa anajiona yeye ni malaika."

(Guide to the Aetiology&Manifestations of desease of Melancholia by Allama Burhanuddin Nafees).

Maono ya ajabu ajabu ya mgonjwa, mara nyingi, hunasiabiana na mambo aliyokuwa

akiyafanya wakati wa uzima wake. Mathalani, kama mgonjwa alikuwa mtu wa dini,

hudai utume na uwezo wa kufanya miujiza, huzungumzia uungu na kuwahubiria watu

mambo hayo." (Askeer-e-Azam Juz 1 uk 188, by Muhammad Aza Khan).

"Kwa mzushi wa ufunuo, iwapo jambo hili linathibitishwa kuwa anasumbuliwa na

Umanyeto, Unyogovu au Kifafa, basi huna haja ya kuhitaji ushahidi mwingine wa

kuukataa utume wake, kwani hili ni pigo ambalo kwalo jengo zima la ukweli

husukumwa mbali na msingi wake". (Na Dkt. Shahanawaz Qadiani in Magazine

Review of Religions, Qadiani Tarehe, Agosti 1926 A.D.).

MIRZA QADIANI NA POMBE + ULEVI WA DAWA ZA KULEVYA

" Afyuni (opium), mara nyingi, hutumika katika Dawa za tiba ambazo Masihi (Mirza

Ghulam Ahmad Qadiani) alikuwa akisema kuwa mbele ya macho ya madaktari,

afyuni ni nusu ya tiba. Hivyo, matumizi ya afyuni kwa tiba na si kwa ulevi hayapingwi

kwa namna yoyote ile. Kila mmoja wetu. kwa kujua au kwa kutojua, ametumia afyuni

kwa kiwango Fulani”.

“Hazrat Masiih Muwuud (Masih Mirza Ghulam Ahmad Qadian aliyeahidiwa) alifanya

tiba ya Tiryaq-e-llahi kwa maelekezo kutoka kwa Mungu na kichanganyio chake kikubwa kilikuwa ni afyuni; na dawa hii, baada ya kuongezewa afyuni, akapewa Hazrat Khalifa (Khalifa wa kwanza Hakiim Nuuruddin), alipewa na (Mirza Qadian)

kwa zaidi ya miezi sita na yeye mwenyewe alikuwa akiitumia wakati wa matatizo ya

maradhi".

(Article by Mian Mahmuud Ahmad Khalifa Qadian in Akber Al Fazal, Qadian, Juz 17 Na 6, Julai 19, 1929).

Pombe ya Toniki

“Ndugu yangu Mohammad Hussein Sahib

Mungu akulinde, Assalam-O-Alaikum

Yar Muhammad Mkuu sasa anatumwa. Vitu vya kununuliwa, nunua wewe

mwenyewe na nunua chupa moja ya Mvinyo ya Toniki Dukani kwa Plommer lakini

mimi nahitaji Mvinyo ya Toniki zingatia hili. Nyingine ni O.K” (Imesainiwa: Mirza Ghulam Ahmad Qadiani)

(Barua za Imam kwa Katibu Mukhtasi. Mkusanyiko wa Barua za Mirza Ghulam

Ahmad Qadiani kwa Hakiim Mohammad Hussein Qadiani, mmiliki wa zahanati Rafiqus-

Sehat Lahore)

"Undani halisi wa Mvinyo ya Toniki ulichunguzwa kutoka dukani kwa Plommer mjini

Lahore kupitia kwa Dkt. Aziz Ahmad aliyeandika jibu hili :

‘Kwa maagizo, nilichunguza Dukani kwa Plommer na jibu ni hili lifuatalo:

"Mvinyo ya Toniki ni aina ya mvinyo kali na ya kulevya ambayo huagizwa kutoka

Uingereza (U.K. Wilayat) katika chupa zilizozibwa. Bei yake ni Rupia 5 Annas 8 (21/9/1933)."

(Sauda-e-Mirza uk. 39 By Hakiim Mohammad Ali, Mkuu wa Chuo, Tibbiya College Amratsar)

Hebu ona jinsi inavyodhihirika kuwa madai ya Mirza kwamba yeye ni Masihi

aliyeahidiwa, Mahdi na Nabii yalikuwa ni dalili za maradhi na hayakutokana na

ufunuo wala mazungumzo na Mungu. Tatizo hili likazidishwa na matumizi ya Afyuni

na Mvinyo ya Toniki. Namuomba MwenyeziMungu awape mwongozo na ufahamu

Makadiani ili wafuate njia sahihi. Vinginevyo wafuasi wa mgonjwa wa unyong’onyevu,

nao pia watakuwa wanyong’onyevu.

Mouvement Anti Ahmadiyya en Islam

Dr Syed Rashid Ali

PO BOX 11560 Dibba, Al Fujairah. U.A.E

E-mail : rasyed@emirates.net.ae/ alhafeez.org/rashd

اضيف بواسطة :   admin       رتبته (   الادارة )
التقييم: 0 /5 ( 0 صوت )

تاريخ الاضافة: 26-11-2009

الزوار: 2154


المقالات المتشابهة
المقال السابقة
Qadianis Hopes Dashed
المقالات المتشابهة
Writings Speak
المقال التالية
Knowledge of Mirza
جديد قسم مـقـالات الموقـــع
القائمة الرئيسية
البحث
البحث في
القائمة البريدية

اشتراك

الغاء الاشتراك