عرض المقال :Part 2..Finality of Prophethood by Maudodi
  الصفحة الرئيسية » مـقـالات الموقـــع » كشف البلية بفضح الأحمدية » Non - Arabic Articles » Swahili

اسم المقال : Part 2..Finality of Prophethood by Maudodi
كاتب المقال: webmaster
yani) kwa jina la Masih Mau’ud, “Masihi aliyeahidiwa” bila shaka ni batili na ni mkakati wa upotoshaji.

Moja kati ya mambo ya kuchekesha ya jumuiya hii ni kuwa Mirza ghulam Ahmad Qadiani ambaye anajiona ndiye mlengwa wa bishara za Sayidina Muhammad ametowa ufafanuzi wa ajabu wa utambulisho wake kama “Isa mwana wa Maryamu”.

“Yeye (Mungu)alinipa jina la Maryamu katika sura ya tatu ya Barah-ini- Ahmadia. Baada ya hapo kama inavyodhihirika katika Barahin-i-Ahmadia nikalelewa kwa sura ya Maryamu kwa miyaka miwili. Kisha mwili wangu ukajazwa roho ya Isa kama vile mwili wa Mariyamu ulivyojazwa roho ya Isa na kwa maana ya kitamathali nikawa mjamzito kwa roho ya Isa. Mwishowe baada ya kipindi cha miezi mingi (zaidi ya miezi kumi), nikageuzwa kutoka Maryamu kuwa Isa kwa ufunuo wa Mungu, ambao umeandikwa mwishoni mwa sura ya nne ya Barahin-i-Ahmadia. Hivyo kwa njiya hii nikawa mwana wa Maryamu”. (Kashti-e-Noah, 87-89).

Kwa maneno mengine kwanza Mirza alikuwa Maryamu, kisha akapata mimba na mwishowe kutoka katika tumbo lake mwenyewe akatokeya kama Isa mwana wa Maryamu. Hata hivyo, kulikuwa na kikwazo kimoja kilichobakiya.

Kwa mujibu wa Hadith, Isa mwana wa Maryamu atatokeya Damascus,mji mashuhuri wa Syria ambao umevuma kwa miyaka elfu kadhaa, hadi leo mji unajulikana kwa jina hili katika ramani ya duniya.

Utata huu ukafafanuliwa na maelezo mengine ya kuchekesha: “Ifahamike kuwa kwa ajili ya ufafanuzi wa neno “Damascus.” MwenyeziMungu amenifafanuliya kwa ufunuo kuwa Hapa jina hilo hilo Damascus limetolewa kwa kijiji ambacho wakazi wake wana sifa za Yazid na ni wafuwasi wa tabiya na mawazo ya Yazid chafu. Mji huu wa Qadian, kwa sababu kuwa wengi wa wakazi wake wana sifa za Yazid kwa tabiya zao, unanasibiyana na una haiba fulani inayofanana na Damascus (Marginal note of Izala-i-Auhma, uk. 63-73).

Lakini hivyo sivyo kabisa, lipo tatizo jingine tena linalohitaji ufafanuzi nalo ni kwamba Hadith zimebashiri kuwa Isa atashuka jirani na Nguzo nyeupe. Tatizo lilitatuliwa pale “Isa mpya” alipojengewa nguzo yenye rangi nyeupe.

Hadith zimetaja kuwa nguzo hiyo nyeupe itasimama kabla ya kushuka kwa Isa jirani nayo lakini kule Qadiani nguzo ilijengwa baada ya kutokeya kwa “Masih Mau’ud. Lakini achiliya mbali tofauti hii. Yeyote asomaye fafanuzi hizo za “Masih Mau’ud” kwa macho safi atafikiya hitimisho kuwa huu ni upotoshaji unapenyezwa waziwazi na mzushi huyu.

Tanbihi

Tanbihi 1

 

Kwa nukta hii wale wanaoukanusha mwisho wa Utume wa Muhammad hutaka kuijuwa Hadith ambayo dai hili limeripotiwa.Swali hili kwa kweli linadhihirisha umbumbumbu wao.Qur’an inatowa majibu ya madai haya ya Mafatani kwa nukta kadhaa bila kulitaja dai lenyewe.Hata hivyo katika kila jibu kila aya husika inatowa ushahidi sahihi juu ya dai linalojibiwa. Kuhusiyana na suwala hili piya jawabu lina sehemu ya swali. Utumizi wa kiunganishi “bali”mwishoni mwa sentensi unaashiriya sehemu ya swali bado haijajibiwa.Hivyo, sentensi ya pili ndiyo inayotowa jibu la sehemu iliyobaki ya swali hilo. Sentensi ya kwanza iliwabainishiya wapinzani jawabu la swali lao kuwa eti “Muhammad alimuowa mkwewe”. Hata hivyo nukta ya pili ya swali kuwa wapi ilitoka shurti kwa Mtume kufanya hivyo bado nayo ilihitaji jibu piya. Jibu hilo likatolewa na sentensi iliyofuwata katika aya hiyo.

 

"Lakini, kwa hakika Muhammad ni Mtume wa MwenyeziMungu na ni Mwisho wa Mitume wa Mungu"

 

Nukta hii yaweza kufafanuliwa zaidi kwa kuchukuliya mfano wa mazungumzo ya kawaida. Mtu anaweza kusema, “Zaid hakuinuka bali Bakari ndiye aliyesimama wima”. Hapo hii inaleta maana kuwa Zaid hakuinuka lakini hii haishii hapo, kwani inazusha swali. Kama Zaid hakuinuka nani basi aliyesimama? “ kifungu cha maneno, bali Bakari ndiye aliyesimama wima ndicho kinachotowa majibu ya swali. Ni vivyo hivyo katika jibu la swali la hilo.

Tanbihi 2

Tumezirejeleya kamusi tatu hapa lakini bado ufafanuzi wa suwala hili hauishii katika makamusi haya tu. Kamusi zote sanifu za lugha ya Kiarabu zinalitafsiri neno Khatam kwa maana hiyo tuliyoitowa. Lakini wale wanaokanusha mwisho wa utume katika jitahada zao za kufanya shambulio la kinyemela dhidi ya dini ya MwenyeziMungu wanadai kuwa kama tutamuelezeleya mtu fulani kama “Mwisho wa Washairi” au “Mwisho wa Wanasheriya” au “Mwisho wa Wafasiri”, si lazima kwamba tuwe na maana kuwa hakuna mshairi au mwanasheriya au mfasiri atakayekuja baada yao, bali tunamaana kuwa sifa zote za utendaji wao zimejikita kwa watu hao. Hata hivyo, maana halisi ni kuwa pale tunapotumiya mifano hii ya kummwagiya sifa mtu fulani bado hatubadilishi au kuondosha maana halisi ya neno “Mwisho”. Ni makosa kudhani kuwa kwa matumizi ya kitamathali yanayoelezeya sifa au ubora wa mtu, ndiyo basi neno “Mwisho” linapotyeza maana yake halisi au maana yake ya asili ambayo ni “hatima”. Dhana kama hiyo yaweza tu kukubalika kwa mtu asiyekuwa na elimu ya msingi ya kanuni za sarufi. Hakuna kanuni ya kisarufi katika lugha yoyote ambapo kwayo maana ya kitamathali ya neno yaweza kuchukuliwa kama maana halisi. Isitoshe, maana ya kitamathali habadilishi au kufuta maana halisi ya neno.

Unapomwambiya Mwarabu, “Ja Khatam ul-Quum” kwa hakika hataichukuliya kauli hii kwa maana ya mtu mtu bora mwenye sifa kubwa katika kabila amekuja. Bali kinyume chake atamaanisha kuwa kabila zima hadi mtu wa mwisho kabisa limekuja.”

Hakuna hoja tena ya kutafakari. Misemo hiyo kama “Mshairi wa Mwisho,” Mwanasheriya wa Mwisho au “ “Msimulizi wa Mwisho wa hadith” ni sifa zinazotumiwa na binadamu kuwasifu wanadamu wenzao ambao wanawaona ni bora na wenye sifa bora.

Wale wanaotumiya misemo hii ya kusifu watu, kwa kweli hawawezi kusema wala kujuwa kuwa watu wenye sifa kama hizo watakuja huko mbele au la. Kwa hiyo kwa wanadamu misemo hii ni ya kutiya chumvi, lakini Mungu anapotumiya sifa fulani imeishiya kwa mtu huyo hakuna sababu ya kuichukuliya kwa maana ya kitamathali kwa usemi wa kibinadamu.. Kama Mungu angemtangaza mtu fulani kuwa ni “Mshairi wa Mwisho”basi kweli mtu huyo angekuwa Mshairi wa mwisho kwa maana ya kiistilahi ya neno hilo. Kama mtu anamteuwa mtu fulani kama mtume wake wa “Mwisho”, hakuna tena uwezekano kwa mtu mwingine yeyote kupata hadhi hiyo baada yake.

Mungu ni Mjuzi wa mambo yote. Lakini binadamu hana isipokuwa elimu ndogo tu. Ikiwa hivyo basi, mtu anawezaje kumaanisha sifa ya mtu kuwa “Mshairi wa mwisho” au “Mwisho wa washairi wote” kwa maana ileile kama Mungu anavyomtangaza mtu kuwa “Mtume wa Mwisho” ?

Tanbihi 3

Wakirejeleya Hadith hii wale wasioamini Mwisho wa utume hudai kuwa Mtume Mtukufu (saw) aliuita msikiti kuwa ni msikiti wa mwisho licha ya ukweli kwamba huo siyo msikiti wa mwisho kwani misikiti chungu tele imejengwa baada ya msikiti huwo duniyani kote. Vivyo hivyo pale mtume mtukufu aliposema: “Mimi ni Mtume wa Mwisho”, haikuwa na maana kuwa mlolongo wa Mitume umekoma, bali Muhammad alikuwa wa mwisho kwa mnasaba wa ubora wake miongoni mwa Mitume wa Mwenyezimungu ambapo hata msikiti wake ulikuwa wa mwisho kwa maana hiyo hiyo. Hoja hiyo ya kipuuzi ni ushahidi usiopingika wa ukweli kuwa watu hawa wamepoteza ule uwezo wa kuelewa maana sahihi ya maneno ya MwenyeziMungu na yale ya Mtuime wake. Hata mtazamo wa juujuu tu kwa njiya ya isinadi ya Hadithi ambazo kwa muktadha wake Hadith hii mahususi imenakiliwa unatowa maana sahihi ya maneno ya Mtume Mtukufu yaliyo wazi kwa mtu yeyote. Kwa muktadha huu Hadith mbalimbali ambazo Imamu Muslim amezikariri kutoka kwa Sayidina Abu Huraira, Sayidina “Abdullah bin” Uma na mama wa waumini bi Maimuna zinasema kuwa kuna misikiti mitatu tu duniyani ambayo inatukuzwa kwa utukufu mkubwa ambapo misikiti hii ndiyo mitukufu zaidi ya misikiti yote. Ibada katika misikiti hii huwa na thawabu kubwa mara elfu kulinganisha na sala inayosaliwa katika misikiti mingine. Ni kwa sababu hii kwamba imehimizwa kisheriya kufunga safari kwenda kusali katika misikiti hii. Hakuna msikiti mwingine wowote ukiondowa hii mitatu, unaoweza kudai utukufu huwo kuwa mtu afunge safari kwenda kusalia huku akiiacha misikiti mingine yote. Miongoni mwa misikiti misikiti mitatu yenye utukufu mkubwa katika Uislamu ni hii; wa kwanza ni Masjid Al-Haram ambao ulijengwa na Nabii Ibrahim (as), wa pili ni “Masjid al-Aqsa” ambao ulijengwa na Nabii Suleiman (as); na wa tatu ni “Masjid-I-Nabawi” mjini madina ambao uliasisiwa na Mtume Muhammad (saw). Maneno ya Mtume mtukufu kuhusiyana na “msikiti wa mwisho” yatazamwe kwa muktadha huu. Maneno ya Mtume yalikuwa na maana kuwa Hakuna Mtume atakayekuja baada yake hivyo hakutakuwa na Msikiti wa nne baada ya Masjid-I-Nabawi (Msikiti wa Mtume wa mwisho).Hivyo, kinachokuja hapa ni kuwa hakuna msikiti mwingine unaopaswa kupata utukufu huo, eti kwamba katika Msikiti ibada ilipwe thawabu nyingi zaidi kulinganisha na misikiti mingine na zaidi ya hivyo hakutakuwa na msikiti wa nne ambao watu, kisheriya au kwa kutaka, watalazimika kufunga safari ili kwenda kusaliya humo.

Tanbihi 4

Kinyume na maneno ya Mtume Mtukufu, wale wanaokanusha Mwisho wa Utume hunukuu maneno yafuwatayo yanayodaiwa kusemwa na Bi Aisha: “Sema, kwa hakika, Mtume Mtukufu ndiye Mtume wa Mwisho wa MwenyeziMungu; lakini usiseme kuwa hakuna mtume atakayekuja baada yake” Kwanza kabisa ni ujasiri wa ajabu kunukuu maneno ya Bi Aisha kupinga hukumu ya wazi ya Mtume. Isitoshe maneno hayo yanayosemekana kusemwa na Bi Aisha hayana uthibitisho. Hakuna kitabu chochote cha Hadith sahihi chenye maneno haya ya Bi Aisha. Wala hakuna mkusanyaji yoyote mashuhuri wa Hadith aliyerekodi au kuirejeleya kauli hiyo. Hadith hii imetolewa katika Tafsiri iitwayo Durr-Manthur na kitabu cha Hadith kijulikanacho kama Takmilah Majma-ul-Bihar, lakini chanzo na ithibati yake havijulikani. Ni kiwango cha juu cha ujasiri kutowa kauli ya Sahaba huyu wa kike wa Mtume ili kuyapinga maneno ya wazi ya Mtume Mtukufu ambayo Muhadithuna mashuhuri wameyasambaza kwa isinadi sahihi.

Tanbihi 5

“Maana ya kuvunja Msalaba” na “Kuuwa nguruwe” ni kuwa Ukristo utafutika. Msingi wa dini ya Ukristo unatokana na imani kuwa Mungu alimsulubisha Mwanawe wa pekee (Nabii Isa as) msalabani na kumfanya afe kifo cha “laana” ili aweze kufidiya dhambi za mwanadamu. Miongoni mwa wafuwasi wa Mitume, Wakristo wao wamejiweka peke yao kwa kuikataa shariya yote ya Mungu na kuishikiliya imani hii tu. Nguruwe aliharamishwa na Mitume wote lakini Wakristo wao wameendeleya tu kuihalalisha.Hivyo, pale Isa (as) atakapotokeya na kutangaza, “Mimi si mwana mwana wa Mungu; Sikufiya msalabani wala sikufuta dhambi za mtu yeyote”, msingi mzima wa imani ya Kikristo hapo utakuwa umebomoka. Vivyo hivyo sifa nyingine pekee ya Wakristo nayo itafutika pale Isa (as) atakaposema; “Sikupata kuhalalisha nguruwe hata kidogo kwa Wafuwasi wangu wala sikuwaweka huru na mipaka ya Shariya ya Mungu”.

Tanbihi 6

Kwa maneno mengine kauli hii ina maana kuwa tofauti kati ya wafuwasi wa dini mbalimbali itafutika na walimwengu wote wataunga undugu wa Kiislamu. Kwa hali hiyo hakutakuwa na sababu tena ya kumtoza kodi ya kidini mtu yeyote. Ufafanuzi huu unaungwa na na Hadith Na 5 na 15.

Tanbihi 7

Maana yake ni kwamba Isa (as) hatakuwa Imamu wa sala. Atasali nyuma ya Imamu aliyepo wa Waislamu.

Tanbihi 8

Maana ya maneno haya ya Isa (as) ni kuwa, “Mtu yeyote miongoni mwenu awe kiongozi wenu.”

Tanbihi 9

Tafadhali zingatiya kuwa Lod (sasa hivi Lyadda) ipo umbali wa maili chache kutoka Tel Aviv, mji mkuu wa dola ya Israili ndani ya Palestina. Wayahudi wamejenga kituwo kikubwa cha anga katika sehemu hii.

Tanbihi 10

Afiq ambayo siku hizi inajulikana kama Fiq ni mji wa Syria uliopo mpakani baina ya Syria na Israil. Kuna ziwa linaloitwa Tabriya maili chache upnde wa magharibi wa mji huo. Ziwa hili ndiyo chanzo cha mto Jordan, upande wa kusini-magharibi wa ziwa hili kuna njiya inayopita katikati ya milima ambayo inateremkiya umbali wa futi elfu mbili hadi katika Ziwa la Tibriya ambako mto unatokeya. Njiya hii ya mlimani inaitwa Kiteremko cha Afiq (the slope of Afiq).

Tanbihi 11

Wale wakanushao uwezekano huu wapitiye aya ya 250 ya Surati Baqara ambapo MwenyeziMungu anasema kwa maneno ya wazi kuwa alimfisha mmoja wa viumbe vyake kwa miyaka miya moja na baada ya muda huo akamfufuwa.

Tanbihi 12

Maumaa wa Kiislamu wamelifafanuwa suwala hili kwa kina. Allama Taftazani (722 A.H. – 792 A.H.) katika Shara “Aqaid-I-Nasafi kaandika: “Imethibitika kuwa Muhammad ni Mtume wa Mwisho... Inaposemwa kuwa kwa mujibu wa Hadith kushuka kwa Isa (as) kutatokeya baada ya Mtume Muhammad sisi tutasema hivi: “Naam, jambo hili limeelezwa katika Hadith. Lakini Isa (as) atatokeya kama mfuwasi wa Muhammad. Shariya ya Isa inabaki katika hali ile ile ya kufutika. Ndiyo kusema kuwa yeye hatapokeya ufunuo wowote kutoka kwa Mungu wala hatasimamisha sheriya yoyote. Katika matendo yake yote atamwakilisha Muhammad tu”.

Jambo hilo limesisitizwa na Allama Alusi katika Tafsir Ruh-al-Ma’ani: Hapo baadae isa atakapotokeya, atakuwa na hadhi kama Nabii wa Zamani. Tangu hapo Kwa hakika Mungu hatomuondosheya hadhi yake hii lakini hatafuwata sheriya ya wakati wake kwa sababu sheriya zote ikwemo yake zinabakiya vile vile katika hali ya kufutika. Hivyo itakuwa amri ya Mungu kwa Isa (as) kufuwata kwa maandishi na kwa imani kazi ya kusimamisha sheriya ya sasa ya Muhammad (saw).

Hatapokeya wahai kutoka kwa Mungu wala hatapewa kazi ya kuleta sheriya mpya ya dini. Katika matendo yake yote, Isa ataishi kama mwakilishi wa wafuwasi wa Muhammad na atafanya kazi kama naibu na mmoja wa watawala wa wafuwasi wa Muhammad (saw).

Imam Raz. anaifafanuwa zaidi nukta hiyo kama hivi:Kipindi cha Utume kiliendeleya hadi alipokuja Mtume Muhammad (saw). Pale Muhammad aliponyanyuliwa kuwa Mtume ndipo kipindi cha kuja kwa Mitume kilipofikiya mwisho. Si jambo lisilofahamika kuwa Isa (as) akishuka atakuwa mfuwasi wa Muhammad (saw).

Tanbihi 13

Ingawaje Hadith mbili (Na 5 na21) zina ushahidi wa kutosha kuwa Isa (as) ataelekeya kuwa kama Imamu katika sala kwanza baada ya kushuka kwake, Hadith chungu mzima ambazo ni sahihi zaidi (pitiya Na3,7,9’15,16) zinauzungumziya ukweli kuwa Isa (as) atakataa kusalisha. Atamtaka Imamu aliyepo kupita mbele na kusalisha. Wanazuwoni wote wa Hadith na Mufasiruna wanakubaliyana juu ya jambo hili.

الصفحات[ 1] [2]
اضيف بواسطة :   admin       رتبته (   الادارة )
التقييم: 0 /5 ( 0 صوت )

تاريخ الاضافة: 26-11-2009

الزوار: 4231


المقالات المتشابهة
المقال السابقة
Part 1..Finality of Prophethood by Maudodi
المقالات المتشابهة
المقال التالية
Jinsi Mirza Ghulam wa Qadiyyan anavyojikanganya katika maandishi yake
جديد قسم مـقـالات الموقـــع
القائمة الرئيسية
البحث
البحث في
القائمة البريدية

اشتراك

الغاء الاشتراك