عرض المقال :Merchant of Qadian
  الصفحة الرئيسية » مـقـالات الموقـــع » كشف البلية بفضح الأحمدية » Non - Arabic Articles » Swahili

اسم المقال : Merchant of Qadian
كاتب المقال: webmaster
ndi juu ya vichwa vyetu, himaya yake idumu. O Qaisariyya e Mubaraka Malkia! Mwenyezi Mungu akulinde, akupe uhai mrefu, heshima na mafanikio, nyoyo zetu zielekee kwako... ni ukweli kwamba nyoyo zinazopendana hukumbukana), Sihitaji kutumia lugha ngumu kuelezea ninavyokupenda katika moyo wangu, moyo umekita mapenzi na  heshima kwako. Dua zetu za usiku na mchana zimeendelea kukutiririkia kama mkondo... ingawa najua kwamba nimetekwa na hisia kali katika moyo wangu, ningepaswa kelezea heshima, utii na shukrani zangu mbele ya Hazoora e Hind, utawala wake uwe daima dumu, lakini siwezi kuelezea shauku ya dhati niliyo nayo”.(Sitara -e-Qaisariyah, Roohan Khazain juzuu ya 15 uk. 111).

“Vitabu nilivyoandika katika kuutukuza utawala wa kiingereza vimesheheni makabati, hasa vile vilivyojaribu kufutilia mbali dhana ya Jihad ambayo waislamu wengi wameishikilia na kuiamini sana. Hili ni jukumu kubwa kwa serikali. Kwa hiyo natumai zawadi nono inayolingana na kazi hiyo”.(Tabligh e Risalat, Vol.7, uk. 19).

Picha halisi ndiyo hii. Jukumu la Mirza lilikuwa kujiingia katika kupiga vita moyo wa Jihad miongoni mwa Waislamu ili wawe watiifu kwa makufari. Alikuwa akimuomba Mwenyezi Mungu adumishe utawala wa serikali ya kikafiri kwa sababu ilikuwa ndio ngao yake. Mirza Ghulam Ahmad alikuwa ndiye wa kwanza kujiita Mtume katika historia ya Uislamu aliyehubiri utwana kwa wafuasi wake. Tukiwaweka kando Mitume wa Allah, hajatokea kiongozi wa nchi yoyote ile iliyependelea utumwa badala ya uhuru kwa nchi yake. Lakini Lahaula! Mirza kwa tamaa ya maslahi ya kidunia, aliuza imani yake na imani ya maelfu ya waliomfuata. Hii ndio maana alipokula kiapo cha utii, moja ya masharti ilikuwa utii kwa serikali ya Uingereza:

“Masharti ya uzinduzi: Nimewasilisha vielezo vya hotuba zangu za muda wa miaka 17...ambazo zinazothibitisha wazi kwamba nimekuwa nikiitakia mema serikali ya uingereza kwa dhati ya roho na moyo wangu..kama nilivyoelekeza mwanzo katika sharti la 4 la uzindui kwamba kwa ukweli kabisa nimekuwa mtiifu kwa serikali ya kiingereza na ni mwenye roho yenye kujali  ubinaadamu”...”(Kitab ul-Bariyyah, Roohan Khazain vol.13 uk.10).

Ukweli huu waweza kuwashangaza wafuasi wengi wa Ahamadiyya wa hivi sasa kwa kuwa wengi wao hawajawahi kusoma vitabu vya Mirza Ghulam Ahmad na elimu yao juu ya mafundisho yake kwa kiasi kikubwa imeegemezwa katika maandiko ya propaganda yanayosambazwa ndani ya jumuiya hiyo. Uthibitisho mkubwa ni mfumo wa kuapa. Kiapo cha asili hivi sasa hakipo. Kiapo cha hivi sasa hakina sharti Na. 4 lililotajwa hapo juu. Limekwenda wapi sharti hilo? Nani aliyeliondoa sharti hilo? Nani anayejaribu kumdanganya nani? Makadiani  waulize maswali haya kwa masheikh(murrabbi) wao.

Dondoo kutoka maisha ya Mirza

Mnamo mwaka 1907 kuelekea mwisho wa uhai wake, Mirza alifanya tathmini ya kazi ya aliyoifa kwa miaka yote na mafanikio aliyoyapata:

“Hakuna anayenijua. Wala hakuna ajuaye kuwa ningaliweza kuja kuishi maisha ya wasaa. Nilivyokuwa navyo ni ilikuwa sehemu ndogo tu ya urithi  katika vijimali alivyoacha baba yangu. Baadaye Mwenyezi Mungu akaniwepesishia kidogo wakati ambapo sikuweza kutegemea kupata walau rupiya 10 kwa mwezi. Hata hivyo Mwenyezi Mungu akaigeuza hali yangu ya maisha na akaniunga. Sasa  nina zaidi ya rupiya laki tatu”(kwa kulinganisha na pesa za sasa hivi rupiya laki tatu ni mamilioni ya dola).(Roohan Khazain, Vo. 22,uk.220-221, Haqeeqat ul-Wahi, uk.211-212, 1907).

“Imekuwa ni wajibu kwetu kubaki tukiishukuru serikali hii tukufu ya Uingereza”.(Iza e Auham, footnote).

“Ushauri wangu kwa Jamaat ni huu, wanapaswa kuufanya himaya ya Kiingereza kama yenye mamlaka juu yao(Uulil Amr) na wabaki kuitii kwa moyo mkunjufu kabisa”.(Zuroorat ul Imam uk.23).

Taratibu za kipesa katika Ahmadiyya ya leo

Waliomfuatia Mirza katika uongozi wa Maqadian walikuwa na utamaduni wa kujali pesa zaidi:

“Ndoa ya Binti wa Amiiril Muuminina, Khalifa wa Masihi al Rabbi(Mirza Tahir), Atiya tul Mujiib(Tooba), Mwenyezi Mungu amlinde, ilifanyika mnamo saa 1.00 usiku uliokuwa wa furaha sana na baraka ndani ya eneo la Msikiti wa AlFazl...si chini ya wageni 600 walihudhuria... kabla ya hapo wakati wa swala za Ijumaa na Alasiri  siku hiyo, Huzoora aliitangaza ndoa hiyo ambayo ilifanyika kwa Muoaji Mukarram Malik Sultan Mohammed Khan Saheb mtoto wa Mukarram Malik Sultan Haroon Khan Saheb kulipa Mahari ya  Rupiya Milioni 1”.(AlFazl International 119 Novemba 1999 mapka 25 Novemba 1999).

Leo hii, kuna kiwango cha moja ya kumi au theluthi moja ya kipato  cha mwezi kinachotakiwa kilipwe na kila mwanachama wa Ahmadiyya kusaidia harakati za kueneza itikadi hiyo. Zaidi ya hivyo, kuna taratibu za aina nyingi za ukusanyaji pesa kwa madhumuni maalum. Profesa Munawaar amendika katika makala yake:

Kuna utoaji na utozaji mkubwa wa pesa katika jumuiya ya Ahmadiyya. Kila Ahmadiyya anapaswa kulipa asilimia 6 ya kipato chake kama CHANDA AAM. Ni malipo ya wajibu, kiasi ambacho hakitalipwa huoneshwa kama deni linalotakiwa kulipwa baadaye kupitia katika akiba yake ya benki. Iwapo Ahmadiyya atakataa kulipa CHANDA, anakoma kuwa mwanachama. Ingawa hiyo CHANDA ni kitu cha hiyari kisicho na kiwango maalum, mwanachama huweza kulipa zaidi kwa kadri ya uwezo wake wakati ambapo ushuru una kiwango maalum na ulipaji wake huwa wajibu, na kiasi kisicholipwa huoneshwa kama salio la deni lisilokwisha abadan.

Mbali ya malipo ya CHANDA AAM, pia kuna malipo mengine ya:

·         ·          CHANDA JALSA SALANA

·         ·          CHANDA TEHREEK JADEED

·         ·          CHANDA WAQF JADEED

·         ·          CHANDA SAD SALA JUBILEE(hii hivi sasaimefutwa)

·         ·          CHANDA KHUDDAMUL AHMADIYYA(CHANDA MAJLIS) ambayo inatakiwaitekelezwe na vijana

·         ·          CHANDA TAMEER HALL(ukumbi huu ulijengwa mwaka 1973 na kumalizika lakini ukusanyaji wa CHANDA hii unaendelea.

·         ·          CHANDA AFRICA

·         ·          CHANDA DISH ANTENA (Ahmadiyya TV Network).

·         ·          CHANDA LAJNA AMA’ALLAH(hii inatozwa wanawake)

·         ·          CHANDA ATFAAL(hii wanatozwa watoto).

·         ·          CHANDA ANSAAR(hii wantozwa watu wazima waliovuka umri wa mika 40).

  

Kwa ufupi, Ahmadiyya anatakiwa kulipa walau asilimia 10 ya kipato chake cha mwezi. Kuna mfumo wa hiyari wa ukusanyaji wa pesa za CHANDA ambazo mkusanyaji hapati sehemu. Ni mfumo ambao haupatikani mahali popote nje ya Ahmadiyya. Mara mbili tatu kwa mwaka wasimamizi tofauti wa CHANDA tofauti huja kutoka vituoni kuhakiki Akaunti ili kuhahakikisha kama kiasi kilichopokelewa kimetumwa(Chanbnagar-Rabwah). Kwa sababu ya mfumo huu, Jamaat inaonekana kama mtandao uliopangwa vizuri kumbe ni shaghalabaghala tupu usiofuata sheria wala kanuni. Jamaat ni kundi lililojiweka vyema katika ukusanyaji wa pesa. Kama kusingalikuwa na mfumo huu mzuri wa CHANDA, leo hii familia za watoto(warithi) wa Mirza Saheb wasingalimiliki maeneo makubwa ya Ardhi(murrabba)(inakadiriwa Murrabba 1 ni sawa eka 25) wala wasingeishi maisha ya anasa na ubadhirifu kama walivyo. Hii ndiyo “Baraka” ya mfumo huu wa pesa za Ahmadiyya). Waahmadiyya wengi huchanga pasi na kujua undani wa michango hiyo.

Rejea

Growing Number of Member in Jamaat Ahmadiyya by Prof. Munnawwar

Email: rsyed@emirates.net.

الصفحات[ 1] [2]
اضيف بواسطة :   admin       رتبته (   الادارة )
التقييم: 0 /5 ( 0 صوت )

تاريخ الاضافة: 26-11-2009

الزوار: 3899


المقالات المتشابهة
المقال السابقة
Mahdi or Messiah
المقالات المتشابهة
Merchant of Qadian part 2
Merchant of Qadian part 1
المقال التالية
Religious Adventurism
جديد قسم مـقـالات الموقـــع
القائمة الرئيسية
البحث
البحث في
القائمة البريدية

اشتراك

الغاء الاشتراك